
25th Sep 2018
By county diary reporter.
Vuta ni kuvute kati ya polisi na wawakilishi wa wadi kaunti ya Murang’a ilitibuka hii leo hatua chache kuigia katika mtaa wa Ndakaini Gatanga.
wakati ambapo viongozi hawa walitaka kuwa na mkutato wa kuhusisha uma katika kutoa maoni yao kuhusiana na pendekezo la kutaka Murang’a ipewe asilimia 25 ya utajiri wa maji ya Murang’a inayoelekea jijini nairobi, swala ambalo lingezungumziwa katika bunge hilo hapo baadae.
Walakini maafisa wa polisi walikuwa gangari eneo hilo tangia nyakati za asubuhi kuzuia mkutano huu, kufuatia fununu kuwa vingozi hawa wangesambaratisha mtiririko wa shughuli ya kupeleka maji haya kwenye jiji kuu.
Polisi walilazimika kutumia vitoa machozi kuwatawanya viongozi hawa na katika harakati hii muwakilishi wa wadi ya Ng’araria Simon Wamwea akashikwa na polisi.
Wamesema kamwe hawalegezi kamba kupigania swala hili, huku nao uma ukiachwa kwenye njia pande wasijue yanayoendelea.