By our reporter
Dereva mmoja wa trela amefariki baada ya kuchomeka kwa kiasi cha kutotambulika baada ya trela lake kugongana ana kwa ana na trela lengine
Ajali hii mbaya zaid ilitokea katika eneo la Kenani kaunti ndogo ya kibwezi kaunti ya Makueni kwenye barabara kuu ya Mombasa Nairobi na kisha magari hayo yakashika moto.
Kamanda wa polisi kaunti ya Makueni Joseph Ole Napeiyan anasema ajali hiyo ilutokea mwendo wa saa kumi na moja asubuhi na trela moja lilikuwa likikwepa shimo lililoko katikati ya barabara hiyo na kugongana na trela lengine magari hayo yakianguka na kuteketea mmoja huyo akiteketea na dereva wa lori la kutoka mombasa akapata majeraha ya kifua.
Napeiyan anasema polisi wangali katika eneo la ajali wakijaribu kutoa mabaki ya aliyefariki sawia na kuhakikisha hakuna mdongamano wa magari.